Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 23:17

Ugonjwa usiojulikana wauwa watu 53 huko DRC


Afisa wa serikali akichukua vipimo vya joto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya mpox huko DRC October 5, 2024. Picha na AFP
Afisa wa serikali akichukua vipimo vya joto wakati wa uzinduzi wa kampeni ya chanjo ya mpox huko DRC October 5, 2024. Picha na AFP

Ugonjwa usiojulukana umeuwa watu zaidi ya 50 huko kaskazini magharibi mwa Congo, kulingana na madaktari wa eneo hilo na shirika la Afya Duniani siku ya Jumatatu.

Muda kati ya kuanza kwa dalili na kifo ni saa 48, kwa idadi kubwa ya visa, na “hicho ndicho kinachotia wasi wasi mkubwa,” Serge Ngalebato mkurugenzi wa huduma za afya katika hospitali ya Bikoro ameliambia shirika la Habari la Associated Press.

Mlipuko huo wa hivi karibuni huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umeanza Januari 21 na visa 419 vimerikodiwa vikiwemo vifo 53.

Kulingana na ofisi ya WHO Afrika, mlipuko wa kwanza ulitokea katika mji wa Boloko baada ya watoto watatu kula popo na kufa katika kipindi cha saa 48 baada ya kupata homa kali.

Forum

XS
SM
MD
LG