Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Septemba 08, 2024 Local time: 03:12

Uchaguzi mkuu Nigeria: Ushindi kwa Tinubu watabiriwa


Mgombea urais wa chama tawala cha All Progressive Congress (APC) Bola Ahmed Tinubu (kulia) na Kashim Shettima wakizungumza wakati wa mkutano wa APC mjini Abuja Julai 20, 2022. Picha na Kola Sulaimon / AFP.
Mgombea urais wa chama tawala cha All Progressive Congress (APC) Bola Ahmed Tinubu (kulia) na Kashim Shettima wakizungumza wakati wa mkutano wa APC mjini Abuja Julai 20, 2022. Picha na Kola Sulaimon / AFP.

Matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais nchini Nigeria wenye utata yanaonyesha mgombea wa chama tawala Bola Tinubu anakaribia kupata ushindi. Shirika la habari la Reuters lilipata matokeo kutoka majimbo 33 kati ya 36 na Abuja, mji mkuu wa serikali yalionyesha hivyo Jumanne.

Ushindi unaotarajiwa wa Tinubu unaendelea kukiweka madarakani chama tawala cha All Progressives Congress katika nchi hiyo mzalishaji mkubwa wa mafuta barani Afrika na yenye watu wengi zaidi duniani. Hata vivyo Tinubu anarithi mlolongo wa matatizo kutoka kwa raisi anayemaliza muda wake.

Huku majimbo manne tu yakiwa yamesalia kutangaza matokeo, Tinubu anaongoza kwa asilimia 34 au kura milioni 7.6 halali zilizo hesabiwa, na kumpa nafasi kubwa ya kutangazwa mshindi Jumanne baada ya uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa wiki.

Vyama vya upinzani vimepinga matokeo hayo ambayo yanatokana na mchakato wenye dosari ambapo ulikumbwa na matatizo mengi ya kiufundi yanayotoakana na kuanzishwa kwa teknologia mpya ya INEC.

XS
SM
MD
LG