Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Oktoba 22, 2024 Local time: 22:29

Polisi Msumbiji wafyatua mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji


Maandamano yaliyoitishwa na mgombea urais Venancio Mondlane nchi nzima kupinga matokeo ya awali ya uchaguzi wa Oktoba 9, huko Maputo, Msumbiji Oktoba 21, 2024. REUTERS/Siphiwe Sibeko
Maandamano yaliyoitishwa na mgombea urais Venancio Mondlane nchi nzima kupinga matokeo ya awali ya uchaguzi wa Oktoba 9, huko Maputo, Msumbiji Oktoba 21, 2024. REUTERS/Siphiwe Sibeko

Kundi la waangalizi wa uchaguzi wa mashirika ya kiraia msumbiji wamesema shambulizi hilo lilitokea katika eneo la Bairro Da Coop karibu na mji mkuu Maputo , na kumuuwa wakili wa chama cha Podemos, Elvino Dias na mwakilishi wa chama paulo Guambe.

Chama kipya cha upinzani Podemos na mgombea wake wa urais Venancio Mondlane wamekataa matokeo ya muda yanayoonyesha uwezekano wa ushindi wa Frelimo chama ambacho kimetawala msumbiji kwa nusu karne , na mgombea wake ni Daniel Chapo.

Venâncio Mondlane akiongea na waandishi wa habari mjini Maputo.
Venâncio Mondlane akiongea na waandishi wa habari mjini Maputo.

Matokeo rasmi yanatarajiwa kutolewa Oktoba 24 lakini kuna wasiwasi kwamba maandamano yanaweza kubadilika na kuwa na umwagaji damu.

Vikosi vya usalama vya msumbiji viliwahi kufyatulia risasi waandamanaji , ikiwemo baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana, hiyo ni kwa mujibu wa makundi ya haki.

Forum

XS
SM
MD
LG