Mto Klamath, unaomwaga maji kutoka Oregon hadi pwani ya California, umesaidia maisha ya binadamu kwazaidi ya miaka elfu moja. Watu wa Yurok na makabila mengine yanayoishi kando ya ukingo wake kwa zaidi ya miaka elfu moja wametegemea mto wa Klamath kama chanzo kikubwa cha mojawapo ya vyakula bora zaidi vya asili: samaki aina ya Salmon.