Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 10, 2024 Local time: 20:42

'Misri kutoka sare na Msumbiji yathibitisha 'ugumu wa mechi' za AFCON'


Mlinzi wa Msumbiji Renildo Mandava (K) akijaribu kumzuia Mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah (10) katika Kombe la Mataifa ya Afrika, kundi B mechi iliyochezwa kati ya Misri na Msumbiji. (Photo FRANCK FIFE / AFP)
Mlinzi wa Msumbiji Renildo Mandava (K) akijaribu kumzuia Mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah (10) katika Kombe la Mataifa ya Afrika, kundi B mechi iliyochezwa kati ya Misri na Msumbiji. (Photo FRANCK FIFE / AFP)

Katika mtanange mwingine, kwenye uwanja wa Felix Houphouet Boigny mjini Abidjan kati ya Misri na Msumbiji nyota wa Mafarao wa Misri Mohamed Salah aliokoa timu yake kutopata kichapo cha aibu.

Hayo yamejiri katika mchezo wao wa ufunguzi siku ya Jumapili wakati Salah alipofunga kwa njia ya penalti katika dakika saba za majeruhi na kuambulia sare ya bao 2-2 dhidi Mamba wa Msumbiji.

Penalti hiyo ilitolewa kufuatia cheki ya VAR baada ya mchezaji wa Misri Mostafa Mohamed kuchezewa faulo katika eneo la hatari na bao la Salah likainyima Msumbiji ushindi wa kwanza wa kihistoria katika michuano ya AFCON.

Ulikuwa mchezo mgumu sana. Nilisikitika kuona wachezaji wangu wakiwa wamechanganyikiwa mwishoni kwa sababu tulistahili ushindi, alisema kocha wa Msumbiji, Chiquinho Conde.

Mohamed alikuwa amewapa rekodi mabingwa mara saba wa Afrika Misri mwanzo mzuri alipofunga bao ndani ya dakika mbili za mchuano wa Kundi B, lakini joto na unyevunyevu vilionekana kuwafanya Mafarao hao kuwa bora zaidi.

Msumbiji, ambao walikuwa hawajashinda mechi katika majaribio 12 ya awali katika mechi nne zilizopita kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika, walisawazisha kupitia Witiness Quembo katika dakika ya 55.

Mchezo huo ulibadilika kabisa wakati Msumbiji walipojipatia bao la pili dakika tatu baadaye wakati Clesio Bauque, aliyeingia kama mchezaji wa akiba katika kipindi cha pili alicharuka na kufanya matokeo kuwa 2-1.

Salah aliokoa Misri, lakini haukuwa mwanzo mzuri wa kampeni yao nchini Ivory Coast ambapo wanajaribu kushinda taji la nane la AFCON na la kwanza tangu mwaka 2010, kabla ya nyota huyo wa Liverpool kuanza kcheza mechi zake za kimataifa.

Nataka kushinda kila mechi ninayocheza na tusiposhinda nahuzunika, lakini hakuna mechi rahisi, alisema kocha wa Misri Rui Vitoria.

Habari hii inatokana na vyanzo mbalimbali vya habari.

Forum

XS
SM
MD
LG