Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 14, 2025 Local time: 00:19

Changamoto ya ulinzi wa Ukraine baada ya Rais Trump kusitisha msaada


Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy katika ofisi ya Oval, Washington, Februari 28, 2025.
Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy katika ofisi ya Oval, Washington, Februari 28, 2025.

Wachambuzi wa siasa katika Umoja wa Ulaya wameonya kwamba itakuwa vigumu sana kwa umoja huo kuziba pengo la msaada wa ulinzi kwa Ukraine baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusitisha msaada huo kwa Kyiv na kuonyesha kuiunga mkono Russia.

Trump amekwenda kinyume na sera ya Marekani kuhusu Ukraine na Russia, na kupelekea majibizano katika white house wiki iliyopita, Trump aliposema kwamba rais wa Volodymyr Zelenskiy alikuwa hana shukran kwa msaada wa Washington.

Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer akutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy mjini London
Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer akutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy mjini London

Hatua ya Marekani kusitisha msaada kwa Ukraine inawashurutisha washirika wa Ulaya wakiongozwa na Uingereza na Ufaransa, ambao viongozi wao walifika white house wiki iliyopita, na wamemkumbatia Zelenskyy wazi wazi tangu alipoondoka White house.
Nchi za Ulaya zinachukua hatua kuimarisha ulinzi wao na kutoa msaada kwa Ukraine, ikiwemo kutafuta namna ya kumaliza vita, japo zinasema bado zinahitaji msaada wa Marekani.
Mkuu wa tume ya Umoja wa Ulaya Ursula Von der Leyen ametangaza mapendekezo ya kuongeza bajeti ya ulinzi ya Ulaya, ambayo anasema inahitaji dola bilioni 840.

Ursula Von der Leyen (Photo by Nicolas TUCAT / AFP)
Ursula Von der Leyen (Photo by Nicolas TUCAT / AFP)


Umoja wa Ulaya unatarajiwa kuandaa mkutano wa dharura Alhamisi, Machi 6.

Forum

XS
SM
MD
LG