Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 22:48

Russia yaendeleza mashambulizi Ukraine


Moscow Jumamosi imesema imeteka vijiji viwili zaidi mashariki mwa Ukraine huku maafisa wa Kyiv wakisema kuwa mashambulizi ya Russia yameua mtu mmoja na kujeruhi 19.

Wizara ya ulinzi ya Russia imesema kuwa vikosi vyake vimekamata Sudne na Burlatske kusini mwa mkoa wa mashariki wa Donetsk.

Miji hiyo iko karibu na mji wa Velyka Novossilka, ambao ulishikiliwa na jeshi la Russia mwishoni mwa Januari.

Jeshi la wanaanga la Ukraine limesema Russia imerusha ndege 154 zisizo na rubani usiku, ambapo 103 kati yao zilitunguliwa na 51 kutoweka kwenye rada bila kusababisha uharibifu au hasara.

Mamlaka za eneo la Ukraine hata hivyo ziliripoti kifo kimoja na majeruhi kadhaa.

Katika eneo la kusini la Odesa, mtu mmoja alikufa na watatu walijeruhiwa, kulingana na waendesha mashtaka wa Ukraine.

Forum

XS
SM
MD
LG