Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 17, 2025 Local time: 15:35

Hunter Biden, mtoto wa Rais Biden, akiri mashtka katika makubalino na idara ya sheria


PICHA YA MAKTABA: Hunter Biden
PICHA YA MAKTABA: Hunter Biden

Mtoto wa rais wa Marekani , Hunter Biden, Jumanne alifikia makubaliano na Idara ya Sheria ya kukiri mashtaka matatu ya kukwepa kulipa kodi na kumiliki silaha kinyume cha sheria, ambayo yanaelezwa kama yanayopunguza uwezekano wake kufungwa gerezani.

Kulingana na kesi iliyowasilishwa mahakamani siku ya Jumanne, Hunter Biden, mwenye umri wa miaka 53, ambaye kwa muda mrefu ametatizwa na uraibu wa mihadarati na uchunguzi wa shughuli zake za biashara nje ya nchi, atakubali mashtaka mawili ya makosa ya kukosa kulipa kwa wakati, kati ya mwaka 2017 na 2018, na kukubali kuwekwa katika hali ya uangalizi, maarufu probation.

Kwa kuongezea, nyaraka za mahakama zilionyesha kwamba Idara ya Sheria ilikubali kutomfungulia mashataka kuhusiana na ununuzi wake wa bunduki mnamo mwaka wa 2018 alipokuwa akitumia dawa za kulevya, ingawa alidai kwenye hati ya ununuzi kuwa hakuwa anatumia dawa hizo.

Makubaliano hayo yanamtaka Biden kusalia bila kutumia dawa kwa miaka miwili na akubali kutomiliki tena bunduki, lakini ni lazima yaidhinishwe na jaji.

Forum

XS
SM
MD
LG