Rais wa Marekani Donald Trump Jumanne alikutana na Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu huko White House kujadili masuala kadhaa, ikiwemo sitisho la mapigano Gaza ambapo Israel ilikuwa katika vita na wanamgambo wa Hamas. Hizi ni baadhi ya nukuu muhimu.
Amri ya Utendaji ni agizo linalotolewa na Rais wa Marekani kusimamia operesheni za serikali kuu. Amri hizi zina nguvu ya kisheria, licha ya kuwa hazihitaji kuidhinishwa na Bunge.
Rais Donald Trump ameanza utawala wake mpya wiki hii kwa kusaini mamia ya amri za kiutendaji kwa masuala mbali mbali kuanzia nishati hadi uhamiaji. Hizi hapa ni baadhi ya amri hizo...
Maandamano yaliyopewa jina la "People's March" yalianza kutoka uwanja wa Franklin na kupita kati kati ya jiji la Washington hadi uwanja mkubwa mbele ya makumbusho ya Lincon.
Wakati utawala wa rais mteule Trump unajumuisha maelfu ya wateuliwa, watu aliowapendekezwa kuunda baraza la mawaziri ni muhimu zaidi.
Muhula wa Madaraka wa Rais wa 39 wa Marekani ulikabiliwa na misukosuko ya ndani na nje ya nchi na pia mafanikio.
Rais wa zamani wa Marekani, Jimmy Carter ambaye alihudumu kwa muhula mmoja tu madarakani kutoka 1977 mpaka 1981, katika kipindi cha urais ambacho kilikuwa na changamoto za uchumi na mzozo wa matekani nchini Iran.
Biden aliwasili Angola Jumatatu kuanza ziara yake iliyokuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu huko Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara na atatumia siku tatu za ziara yake kukabiliana na ushawishi wa China kwa kutangaza mradi wenye matarajio makubwa wa reli unaofadhiliwa na Marekani.
Rais mteule wa Marekani Donald Trump akiwashukuru wafuasi wake baada ya kuchaguliwa na wananchi kuwa rais wa 47. Trump alikuwa na ujumbe wa kujenga umoja kwa wale waliohudhuria mkusanyiko huo wa mkesha wa matokeo ya uchaguzi huko Florida, Marekani.
Tim Walz, gavana wa Minnesota, amechaguliwa kuwa mgombea mwenza wa Makamu wa Rais Kamala Harris katika kinyang’anyiro cha kuwania urais. Hizi ni baadhi ya taarifa kuhusu mgombea makamu wa urais kwa tiketi ya Demokratiki. #us #harris #vp #pick #tim #walz #voaswahili
Rais wa Marekani Joe Biden na Rais wa zamani wa Marekani na mgombea urais kwa tiketi ya chama cha Republikan Donald Trump wakishiriki katika mdahalo wa CNN wa wagombea urais wa uchaguzi wa mwaka 2024 katika studio za Kituo cha Televisheni cha CNN huko Atlanta, Georgia, Juni 27, 2024.
Maadhimisho ya Kumbukumbu ya siku 100 za mauaji ya kimbari yakiendelea huko Kigali, Rwanda. Picha zote kwa hisani ya Ikulu ya Kigali.
Pandisha zaidi