Mwandishi wa Korea Kusini Han Kang mshindi wa tuzo ya Nobel uandishi wa fasihi

(FILES) Korean author Han Kang poses for a photograph with her book The Vegetarian at a photocall in London on May 15, 2016, ahead of the announcement of the winner of the 2016 Man Booker International Prize.

Mwandishi wa Korea Kusini Han Kang amepewa tuzo ya Nobel katika uandishi wa fasihi kutokana na mashairi yake yanayoangazia uhalisi wa kihistoria na kufichua matatizo ya maisha yanayomkumba binadamu.

Riwaya yake ya "The Vegetarian" ilishinda tuzo ya kimataifa ya Booker mwaka 2016.

Han Kang

Mwandishi huyo ni wa 221 kupewa tuzo hilo yenye thamani kubwa sana katika ulimwengu wa fasihi.

Tuzo ya Nobel ya fasihi imekuwa ikitolewa tangu mwaka 1901

Kwa muda wa miongo kadhaa iliyopita, tuzo ya Nobel kwa ajili ya waandishi ilikuwa ikishindwa na wazungu.

Lakini sasa wasio wazungu wamekuwa wakishinda, ikiwemo kutoka Misri, Nigeria, Mexico, Japan na Marekani.