Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 13:42

Wimbi jipya la Eboa laripotiwa Uganda


Picha ya mji mkuu wa Uganda wa Kampala.
Picha ya mji mkuu wa Uganda wa Kampala.

Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika ,(CDC Africa) kimesema Alhamisi kwamba wimbi jipya la maambuziki ya Ebola limezuka Uganda na kwamba juhudi zinafanywa ili kuongeza ufuatiliaji wa maambukizi.

Uganda ilitangaza ugonjwa huo hatari kuwa janga Januari, kwenye mji mkuu wa Kampala kufuatia kifo cha muuguzi mwanamme kwenye hospitali kuu nchini humo. Mgonjwa wa pili aliyefariki ni mtoto wa umri wa miaka minne kulingana na Shirika la Afya Duniani, WHO, likitaja wizara ya Afya ya Uganda.

Ngashi Ngongo ambaye ni afisa wa CDC aliwaambia wanahabari kwamba baada ya kutoa taarifa za hali Alhamisi, tayari kesi tatu za maambukizi zimeripotiwa wakati nyingine mbili zikisubiriwa kuthibitishwa. Ngongo aliongeza kusema kwamba wilaya mbili mpya zimeripoti kesi za Ebola na kwamba kwa ujumla Uganda imeripoti kesi 14 za maambukizi na vifo viwili tangu kuzuka kwa ugonjwa huo, kulingana na CDC.

Ugonjwa unaofanana na Ebola wa Marburg uliripotiwa kwenye nchi Jirani ya Tanzania Januari mwaka huu.

Forum

XS
SM
MD
LG