Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 30, 2025 Local time: 21:52

Waziri mkuu wa DRC asema zaidi ya watu 7,000 wameuawa mashariki mwa nchi


Waziri mkuu wa DRC Judith Suminwa Tuluka
Waziri mkuu wa DRC Judith Suminwa Tuluka

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Jumatatu alisema kwamba “zaidi ya watu 7,000” wameuawa mashariki mwa nchi tangu mwezi Januari, wakati waasi ambao inasemekana wanaungwa mkono na Rwanda walipoteka miji miwili mikubwa.

Wapiganaji wa M23 walichukua udhibiti wa Bukavu, mji mkuu wa jimbo la Kivu Kusini wiki iliyopita, baada ya kuuteka mji mkuu wa jimbo la Kivu Kaskazini wa Goma mwishoni mwa mwezi uliopita.

“Hali ya usalama mashariki mwa DRC imefikia viwango vya kutisha, “ waziri mkuu Judith Suminwa Tuluka aliliambia Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za binadamu mjini Geneva, akisema tangu Januari, “ vifo vya zaidi ya wananchi wetu 7,000” viliripotiwa.

AFP haikuweza kuthibitisha idadi hiyo.

Forum

XS
SM
MD
LG