Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Septemba 09, 2024 Local time: 09:02

Wanaharakati 18 wafunguliwa mashtaka ya kuvuruga usalama nchini Zimbabwe


Rais wa Zimbabwe Emerson Mnangagwa
Rais wa Zimbabwe Emerson Mnangagwa

Polisi wa Zimbabwe wamewafungulia mashtaka wanaharakati 18 walioshiriki maandamano ya kutaka kiongozi mkuu wa upinzani aachiliwe huru, huku serikali ikionya kukabiliana na maandamano kabla ya mkutano wa kikanda.

Watu hao walikamatwa Jumatano wakati Zimbabwe inajiandaa kuwa mwenyeji wa mkutano wa jumuia ya maendeleo ya ma dola ya kusini mwa Afrika (SADC) tarehe 17 Agosti na mkutano wa mwanzo kuhusu biashara na maendeleo ukiwa unafanyika.

Wanne kati ya wanaharakati hao waliondolewa ndani ya ndege kwenye uwanja wa kimataifa wa Harare siku ya Jumatano, chama cha mawakili wa Zimbabwe kilisema.

Wengine 14 walikamatwa katika mji mdogo wa kaskazini magharibi wa Kariba, chama hicho cha mawakili kilisema kwenye mtandao wa X.

Walishtakiwa Alhamisi chini ya sheria za kuvuruga usalama wa umma baada ya kushiriki katika maandamano ya kuomba kuachiliwa huru kwa kiongozi wa upinzani, Jameson Timba ambaye yuko kizuizini tangu mwezi Juni.

Forum

XS
SM
MD
LG