Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Julai 04, 2024 Local time: 08:28

Wafanyakazi wawili wa shirika la misaada wauawa mashariki mwa DRC


Ramani ya DRC
Ramani ya DRC

Wafanyakazi wawili wa shirika la misaada lenye makao yake Uingereza la Tearfund waliuawa katika shambulizi dhidi ya msafara wao mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, shirika hilo la hisani lilisema Jumatatu.

Wafanyakazi hao walikuwa wanasafiri kwa barabara kutoka mji wa Lubero kuelekea Butembo katika eneo lenye vita katika jimbo la Kivu Kaskazini wakati waliposhambuliwa Jumapili wakiwasili Butembo, Tearfund ilisema katika taarifa bila kutoa maelezo zaidi.

Makundi mengi yenye silaha yanashindania ushawishi na rasilimali katika eneo lenye utajiri wa madini la Kivu Kaskazini, ambalo pia limekuwa likipambana na uasi kwa zaidi ya miaka miwili ambao umezidisha mzozo wa kibinadamu, huku zaidi ya watu milioni 2.7 wakihamishwa kwenye makazi yao ndani ya jimbo hilo.

Kiongozi wa eneo hilo Alain Kiwewa amethibitisha kuwa msafara wa shirika hilo ulishambuliwa na kusema magari yake matano yalichomwa. Lakini hakusema nani alihusika na shambulizi hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG