Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Julai 03, 2024 Local time: 16:54

Vyama vya wafanyakazi nchini Nigeria vyasitisha mgomo wa nchi nzima


Maandamano ya vyama vya wafanyakazi Nigeria
Maandamano ya vyama vya wafanyakazi Nigeria

Viongozi vya vyama vya wafanyakazi nchini Nigeria Jumanne walisitisha mgomo wa nchi nzima kuruhusu mazungumzo ya kuongezewa mshahara, baada ya mgomo wao kudumaza safari za ndege, kufunga mtambo wa umeme nchini kote na kufunga ofisi za umma na shule.

Wito wa kusitisha mgomo huo ulitolewa na vyama viwili vikuu vya wafanyakazi, the Nigeria Labour Congress (NLC) na Trade Union Congress (TUC), na mgomo umesimamishwa wakati taifa hilo lenye watu wengi zaidi barani Afrika likikabiliwa na mfumko mkubwa wa bei na sarafu ya naira isiyokuwa imara.

Jumatatu, wafanyakazi wa vyama vya wafanyakazi walifunga mtambo wa umeme wa kitaifa, walidumaza safari za ndege za ndani na kufunga ofisi nyingi za serikali, bandari, vituo vya mafuta ya petroli na mahakama ili serikali itosheleze ombi lao la kuongeza kima cha mshahara.

Serikali baadaye Jumatatu ilisema vyama vya wafanyakazi vimekubali wiki nyingine ya mazungumzo ili kujaribu kufikia makubaliano.

Baada ya mashauriano kuhusu msimamo wa serikali na wanachama wao Jumanne, NLC na TUC walisema wameomba mgomo usitishwe kwa siku saba.

Forum

XS
SM
MD
LG