Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 06, 2024 Local time: 04:13

Tume ya majadiliano nchini Senegal yapendekeza uchaguzi wa rais ufanyike mwezi Juni


Rais wa Senegal Macky Sal akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa majadiliano ya kitaifa, Februari 26, 2024.
Rais wa Senegal Macky Sal akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa majadiliano ya kitaifa, Februari 26, 2024.

Tume ya majadiliano ya kitaifa ya Senegal itapendekeza uchaguzi wa rais ulioahirishwa ufanyike tarehe 2 Juni huku Rais Macky Sall akisalia madarakani hadi mrithi wake atakapoapishwa, mjumbe wa tume hiyo Ndiawar Paye alisema Jumanne.

Taifa hilo la Afrika Magharibi lilitumbukia katika mzozo wa kisiasa ambao haujawahi kutokea baada ya Sall kuahirisha uchaguzi ambao awali ulipangwa kufanyika Februari 25.

Pendekezo la tarehe mpya ya uchaguzi linafuatia siku mbili za mazungumzo yaliyoandaliwa na Sall ili kupunguza mvutano.

Mpango wake na ule wa bunge wa kuahirisha uchaguzi wa Februari 25 kwa kipindi cha miezi 10 ulichochea machafuko.

Pendekezo hilo litawasilishwa kwa Sall ambaye atafanya maamuzi ya mwisho, Paye aliiambia Reuters.

Mazungumzo hayo yaliyofanyika mjini Dakar yalisusiwa na wapinzani wengi, baadhi yao wakitaka uchaguzi ufanyike kabla ya muhula wa Sall kumalizika hapo tarehe 2 Aprili.

Forum

XS
SM
MD
LG