Kundi la Al-Shabaab lenye uhusiano na Al-Qaeda limekuwa likipambana na serikali kuu ya Somalia kwa zaidi ya miaka 15, kujaribu kuweka utawala wa sheria ya Kiislamu katika nchi hiyo maskini.
“Zaidi ya wanamgambo 70 wenye itikadi kali waliangamizwa katika juhudi za pamoja za jeshi la taifa na vikosi vya ndani,” wizara hiyo ilisema katika taarifa.
Operesheni hiyo ilifanyika Jumanne katika maeneo kadhaa ya jimbo la Hirshabelle, kusini mwa Somalia, wizara hiyo iliongeza.
Shirika la habari la AFP halikuweza kuthibitisha idadi hiyo ya vifo lakini mashahidi kadhaa wamethibitisha mapigano hayo.
Forum