Robert Menendez, mwenye umri wa miaka 71, Mdemocrat kutoka jimbo la New Jersey, alikutwa na hatia ya ulaghai, kutatiza kazi ya vyombo vya sheria na kupokea hongo ili kuwapendelea wafanyabiashara wenye uhusiano na Misri na Qatar.
“Mahali fulani njiani, umepotea njia,” Jaji Sidney Stein alisema akitangaza hukumu ya kifungo cha miaka 11.
“Badala ya kufanya kazi kwa manufaa ya umma, ilibadilika kufanya kazi kwa ajili ya manufaa yako.”
Menendez, ambaye alihudumu kama mwenyekiti wa Kamati ya masuala ya kigeni katika Baraza la Seneti, aliapa kukata rufaa dhidi ya uamuzi uliotolewa Julai 2024, na Jumatano alimuomba msamaha jaji huyo kabla ya hukumu dhidi yake.
Forum