Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Aprili 02, 2025 Local time: 21:30

Rais wa Liberia awasimamisha kazi maafisa 457 wa serikali


Rais wa Liberia Joseph Boakai akitoa hotuba baada ya kuapishwa, Monrovia, Januari 22, 2024. Picha ya Reuters.
Rais wa Liberia Joseph Boakai akitoa hotuba baada ya kuapishwa, Monrovia, Januari 22, 2024. Picha ya Reuters.

Rais wa Liberia Joseph Boakai, ambaye aliahidi kupambana na ufisadi uliokithiri, Jumatano aliwasimamisha kazi zaidi ya maafisa 450 wa serikali walioteuliwa kwa kushindwa kutangaza wazi mali zao.

Tume ya Liberia ya kupambana na ufisadi (LACC) iligundua maafisa 457, akiwemo waziri anayesimamia bajeti pamoja na mabalozi, kuwa hawakutangaza mali zao kabla ya tarehe ya mwisho ya mwezi Novemba, kama inavyoagizwa na kanuni za maadili za nchi kwa maafisa wa serikali.

Maafisa hao “wamesimamishwa kwa kipindi cha mwezi mmoja bila malipo hadi watakapowasilisha nyaraka zinazohitajika”, ofisi ya rais ilisema.

Sheria ya Liberia inawataka watumishi wa umma kutangaza mali zao wanapoingia au kuondoka kwenye nyadhifa zao.

Forum

XS
SM
MD
LG