Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 06, 2024 Local time: 23:23

Raia wanne wa China wauawa na wanamgambo mashariki mwa DRC


Milima ya wilaya ya Djugu katika jombo la Ituri, kaskazini mashariki mwa DRC
Milima ya wilaya ya Djugu katika jombo la Ituri, kaskazini mashariki mwa DRC

Shambulio la wanamgambo kwenye mgodi wa dhahabu katika jimbo la Ituri liliwaua raia wanne wa China kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, kulingana na vyanzo vya eneo hilo.

Raia kadhaa wa Congo waliuawa pia au kujeruhiwa katika shambulio hilo, ambalo baadhi ya vyanzo vya eneo hilo vinasema lilifanywa na kundi la wanamgambo la Codeco, wanaodai kulinda maslahi ya kabila la Walendu dhidi ya kabila hasimu la Wahema.

Mashambulizi kwenye migodi na dhidi ya misafara ni jambo la kawaida huko Ituri na kadhalika kusini katika jimbo lingine lenye utajiri wa dhahabu la Kivu Kusini, ambako kuna wachimba migodi wengi raia wa China.

Mizozo juu ya dhahabu kati ya wakazi wa Congo na wachimba migodi raia wa China ni jambo la kawaida.

“Codeco ilifanya shambulio kwenye mgodi wa Wachina” sio mbali na mji wa Abombi katika wilaya ya Djugu, naibu gavana wa jimbo la Ituri Jean Pierre Bikilisende ameiambia AFP.

“Tuna idadi ya awali ya Wachina wanne waliouawa na wanajeshi wawili wa FARDC waliojeruhiwa,” aliongeza.

Vyanzo vingine vya eneo hilo vimesema raia sita wa China ndio waliuawa, vile vile walinzi wao, wanajeshi wawili wa Congo na raia wawili waliuawa.

Forum

XS
SM
MD
LG