Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Oktoba 07, 2024 Local time: 08:24

Papa Francis kuwateua makadinali wapya 21


Papa Francis akiongoza ibada ya misa ya kuombea amani katika kanisa la Santa Maria mjini Roma, Oktoba 6, 2024. Picha ya AFP
Papa Francis akiongoza ibada ya misa ya kuombea amani katika kanisa la Santa Maria mjini Roma, Oktoba 6, 2024. Picha ya AFP

Papa Francis atawateuwa makadinali wapya 21 kutoka duniani kote, alisema hayo Jumapili, katika hatua ambayo haikutarajiwa kushawishi kundi hilo lenye nguvu la watu wa kanisa ambao siku moja watamchagua mrithi wake.

Hafla ya kuwaidhinisha wateule wapya, inayojulikana kama consitory, itafanyika tarehe 8 Disemba, Papa huyo mwenye umri wa miaka 87 alisema wakati wa ibada ya alasiri ya kila wiki na mahujaji na watalii katika eneo la Mtakatifu Petro.

Itakuwa hafla ya 10 kuitishwa na Papa tangu kuchaguliwa kwake miaka 11 iliyopita, kama Papa wa kwanza kutoka Amerika Kusini.

Makadinali hao wapya ni kutoka nchi tofauti ikiwemo Argentina, Brazil, Chile, Peru, Italy, Uingereza, Serbia, Japan, Indonesia, Canada, Ivory Coast na Algeria.

20 kati yao wana umri wa chini ya miaka 80 na watapiga kura katika kongamano kumchagua papa mpya baada ya kifo cha Francis au kujiuzulu kwake.

Mmoja kati ya kundi hilo ana umri wa miaka 99, ni Askofu kutoka Italy. Askofu Mykola Bychok wa Kanisa Katoliki la Ukraine, ana umri wa miaka 44, atakuwa kadinali wa kwanza mwenye umri mdogo.

Forum

XS
SM
MD
LG