Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Julai 01, 2024 Local time: 21:18

Niger imefuta leseni kwa kampuni ya nyuklia ya Ufaransa


Kiongozi wa kijeshi wa Niger, Jenerali Abdourahmane Tchiani
Kiongozi wa kijeshi wa Niger, Jenerali Abdourahmane Tchiani

Niger imefuta leseni ya kufanya kazi ya mzalishaji wa mafuta ya nyuklia wa Ufaransa, Orano, katika migodi mikubwa zaidi ya uranium duniani, kampuni hiyo ilisema Alhamisi, katika hatua inayoonyesha wazi mvutano kati ya Ufaransa na utawala wa kijeshi wa nchi hiyo ya Afrika Magharibi.

Orano imesema imeondolewa kwenye mgodi wa Imouraren kaskazini mwa Niger ambao una takriban tani 200,000 za chuma, zinazotumiwa kwa ajili ya nishati ya nyuklia na silaha.

Uchimbaji wa madini ulitarajiwa kuanza kwenye mgodi huo wa Imouraren mwaka 2015, lakini shughuli hiyo ilisitishwa baada ya kuporomoka kwa bei ya uranium ulimwenguni kufuatia janga la nyuklia ya Japan mwaka 2011.

Serikali ya Niger haikutoa maelezo mara moja kuhusu taarifa ya kampuni hiyo. Lakini ilikuwa imeapa kusahihisha mikataba ya uchimbaji madini nchini na wizara ya madini ilikuwa imeonya kwamba itaipokonya leseni kampuni ya Orano, ikiwa shughuli ya uchimbaji itakuwa haijaanza kufikia Juni 19.

Wiki moja kabla ya tarehe ya mwisho, Orano iliiambia AFP kwamba “kazi ya maandalizi ilikuwa imeanza hivi karibuni huko Imouraren.

“Orano inazingatia uamuzi wa mamlaka ya Niger kufuta leseni yake kufanya kazi kwenye mgodi chini ya kampuni mama ya Imouraren SA,” kampuni hiyo ilisema katika taarifa Alhamisi.

Forum

XS
SM
MD
LG