Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Machi 31, 2025 Local time: 06:16

Mrithi wa waziri mkuu wa Canada achaguliwa na chama cha Liberal


Mark Carney, mrithi wa waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau. Picha ya Reuters
Mark Carney, mrithi wa waziri mkuu wa Canada Justin Trudeau. Picha ya Reuters

Mark Carney, ambaye hivi karibuni atakuwa waziri mkuu mpya wa Canada, ni gavana wa zamani wa benki kuu ya Canada na ile ya Uingereza, atakabiliwa na kibarua kigumu cha kuiongoza Canada chini ya ushuru wa ziada uliowekwa na Rais Donald Trump.

Chama cha Waliberal kimemtangaza Carney kama mrithi wa Trudeau Jumapili baada ya wanachama kumpigia kura katika uchaguzi wenye ushindani.

Trudeau alijuzulu mwezi Januari kufuatia umaarufu katika utendaji kazi wake kushuka sana baada ya karibu muongo mmoja akiwa madarakani.

Carney mwenye umri wa miaka 59 sio mwanasiasa na hajawahi kuwa na wadhifa wowote serikalini, jambo ambalo kwa kawaida lingemuondoa kwenye kinyang’anyiro nchini Canada. Lakini kujitenga kwake na Trudeau na wasifu wake kama mfanyakazi wa benki wa muda mrefu kulimsaidia, na Carney amedai kuwa yeye ndiye mtu pekee aliye tayari kumdhibiti Trump.

Forum

XS
SM
MD
LG