Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Oktoba 19, 2024 Local time: 17:17

Mjumbe wa UN apendekeza Sahara Magharibi ipewe uhuru wake na Morocco


Mjumbe maalum wa UN kwa ajili ya Morocco, Staffan de Mistura. Picha ya maktaba.
Mjumbe maalum wa UN kwa ajili ya Morocco, Staffan de Mistura. Picha ya maktaba.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Sahara Magharibi, Staffan de Mistura ametoa wazo la kugawanywa kwa eneo hilo kati ya Morocco na Polisario Front, kama hatua ya kumaliza mzozo uliodumu kwa karibu miongo mitano

Mzozo huo ulioanza 1975 ni kati ya Morocco inayochukulia Western Sahara kuwa himaya yake na kundi la Polisario Front, linaloungwa mkono na Algeria, likiitisha kujitawala. Morocco kwa upande wake inasema kuwa inaweza tu kuruhusu eneo hilo kujitawala likiwa chini ya serikali yake, lakini Polisario Front limekuwa likiitisha kuwe na kura ya maoni kuelekea kujitawala kama nchi huru.

Wakati akizungumza faraghani mbele ya Baraza la Usalama la UN, de Mistura ambaye ni mwanadiplomasia wa siku nyingi kutoka Italy alisema kuwa ugawanyaji huo utaruhusu kubuniwa kwa taifa huru upande wa kusini, na kwa upande mwingine kuruhusu Morocco kuchukua sehemu iliyobaki ikitambuliwa kimataifa.

Aliongeza kusema kuwa licha ya pendekezo hilo. Wote Morocco na Polisario Front hawakuridhia. Alisema kuwa Katibu Mkuu wa UN anahitaji kutadhimini tena jukumu lake kama mjumbe maalum iwapo hakuna hatua zitakazokuwa zimepigwa kuelekea sululosho la mzozo huo ndani ya miezi 6.

Forum

XS
SM
MD
LG