Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 07, 2024 Local time: 05:16

Mitandao kote duniani yakumbwa na matatizo


Hali ilivyokuwa katika uwanja wa ndege wa Milwaukee, Wisconsin, wakati tatizo la mitandao lilipotokea Julai 19, 2024.
Hali ilivyokuwa katika uwanja wa ndege wa Milwaukee, Wisconsin, wakati tatizo la mitandao lilipotokea Julai 19, 2024.

Mashirika ya ndege, benki, vituo vya televisheni na biashara nyingine duniani kote zilikuwa zikijitahidi kukabiliana na mojawapo ya matatizo makubwa zaidi ya kimtandao katika miaka ya hivi karibuni leo Ijumaa, ambayo yanaonekana kusababishwa na jaribio la kuimarisha programu ya kuzuia virusi.

Mashirika makubwa ya ndege ya Marekani hapo awali yalisitisha safari zote za ndege kutokana na changamoto za mawasiliano -- ingawa kampuni ya American Airlines baadaye ilisema kuwa imerejesha safari zake.

Viwanja vya ndege kote ulimwenguni vilisema mifumo ya kompyuta ilikuwa ikikumbwa na matatizo, na kupelekea ucheleweshwaji wa huduma za safari za ndege.

Kampuni ya Microsoft ilisema kwenye tovuti yake kwamba matatizo yalianza siku ya Alhamisi, yakiathiri watumiaji wa huduma ya Azure inayoendesha programu ya usalama wa mtandao ya CrowdStrike Falcon.

Forum

XS
SM
MD
LG