Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Septemba 17, 2024 Local time: 06:05

Mazishi ya kiongozi wa Hamas yafanyika Doha


Watu wahudhuria sala ya jeneza ya miili ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh na mlinzi wake huko Qatar.
Watu wahudhuria sala ya jeneza ya miili ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh na mlinzi wake huko Qatar.

Mazishi ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh na mlinzi wake yamefanyika mjini Doha leo Ijumaa baada ya kuuawa kwao, kulikowashangaza wengi mjini Tehran siku ya Jumatano.

Hakuna aliyedai mara moja kuhusika na shambulio hilo, lakini tuhuma haraka ziliikumba Israel, ambayo ilikuwa iliapa kumuua Haniyeh na viongozi wengine wa Hamas kufuatia shambulio la kundi hilo la Oktoba 7, mwaka jana, dhidi ya Israeli, ambalo lilizua vita.

Mauaji ya Haniyeh mjini Tehran na shambulizi dhidi ya kamanda mkuu wa kundi la Hezbollah, Fouad Shukur, huko Beirut, yanaweza kuathiri juhudi za kupunguza mzozo wa Mashariki ya Kati, huku Iran pia ikitishia kujibu baada ya shambulio lililofanyika katika eneo lake.

Jeshi la Israel lilisema Alhamisi kwamba lilithibitisha kwamba mkuu wa tawi la kijeshi la Hamas, Mohammed Deif, aliuawa katika shambulio la anga huko Gaza mwezi Julai.

Forum

XS
SM
MD
LG