Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Oktoba 07, 2024 Local time: 08:23

Maandamano ya kuunga mkono Palestina na Israel yafanyika duniani kote mkesha wa maadhimisho ya shambulizi la Oktoba 7


Mtoto akishikilia bendera ya Palestina huju akiwasha mshuma wakati wa maandamano ya kuunga mkono Palestina kabla ya maadhimisho ya shambulizi la Hamas la Oktoba 7 dhidi ya Israel. Picha ya AFP
Mtoto akishikilia bendera ya Palestina huju akiwasha mshuma wakati wa maandamano ya kuunga mkono Palestina kabla ya maadhimisho ya shambulizi la Hamas la Oktoba 7 dhidi ya Israel. Picha ya AFP

Umati wa watu Jumapili ulishiriki katika maandamano ya kuunga mkono Palestina na Israel na hafla za kumbukumbu zimefanyika kote duniani katika mkesha wa maadhimisho ya kwanza ya mashambulizi ya Hamas dhidi ya Israel.

Matukio hayo ya Jumapili yanafuatia maandamano makubwa ambayo yalifanyika Jumamosi katika miji kadhaa ya Ulaya, ikiwemo London, Berlin, Paris na Rome.

Matukio mengine yanapangwa wiki hii, makubwa zaidi yakitarajiwa leo Jumatatu, tarehe ya maadhimisho.

Huko Australia, maelfu ya watu waliandamana Jumapili kuunga mkono Wapalestina na Lebanon katika miji tofauti, huku maandamano ya kuiunga mkono Israel yakifanyika katika mji wa Melbourne.

Forum

XS
SM
MD
LG