Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Septemba 28, 2024 Local time: 06:22

Kauli mbiu ya Siku ya Ukimwi Duniani 2023 ni 'Tuziache Jamii Ziongoze'


White House nchini Marekani yaungana na nchi zote duniani kuadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani.
White House nchini Marekani yaungana na nchi zote duniani kuadhimisha Siku ya Ukimwi Duniani.

Desemba mosi kila mwaka, Shirika la Afya Duniani (WHO), pamoja na jamii na washirika huadhimisha  Siku ya Ukimwi Duniani. Mwaka huu 2023 kauli mbiu ni “Tuziache jamii ziongoze”.

Jamii mbalimbali ambazo zinaishi na kuaathiriwa na, HIV, mitandao ya wananchi kutoka jamii muhimu na viongozi wa vijana wamekuwa na wanaendelea, na umuhimu kwa maendeleo ya kupambana na HIV.

Wanatoa mbinu muhimu za kuzuia, kupima na huduma za matibabu, kujenga uaminifu, kutoa suluhu za njia mbalimbali za ubunifu, kuhamasisha afya, na kufuatilia utekelezaji wa sera na programu mbalimbali na kuwawajibisha wale wanaotoa huduma hizo.

Dunia inaweza kumaliza Ukimwi kwa jamii na kuongoza njia.

Ndiyo maana kauli mbiu ya Siku ya Ukimwi Duniani mwaka huu ni ‘Tuziache jamii ziongoze”, na zaidi ya maadhimisho ya mafanikio mbalimbali ya jamii hizi, ni wito wa hatua kuchukuliwa kuwezesha na kuzisaidia jamii mbalimbali katika nafasi zao za uongozi.

Chanzo cha habari hii ni Shirika la Afya Duniani (WHO).

Forum

XS
SM
MD
LG