Ni wakati Rais wa Marekani Donald Trump akifanya juhudi za kufikia amani.
Kufikia sasa, Baraza hilo lenye wanachama 15 lilikuwa limeshindwa kuchukua hatua yoyote kuhusu mzozo wa Ukraine kwa sababu Russia ina kura ya turufu.
Azimio la MareKani lilipata kura 10 za kuliunga mkono, huku Ufaransa, Uingereza, Denmark, Ugiriki na Slovenia zikijizuia kutoa msimamo.
“Azimio hili linatuweka kwenye njia ya amani. Ni hatua ya kwanza, lakini muhimu, ambayo sote tunapaswa kujivunia,” kaimu Balozi wa Marekani kwenye Umoja wa Mataifa Dorothy Shea aliliambia Bazara hilo.
“Sasa ni lazima tuitumie kujenga mustakabali wa amani kwa Ukraine, Russia na Jumuia ya Kimataifa.”
Forum