Takriban wanakijiji 16 waliuawa na wengine 20 walitekwa nyara kaskazini mashariki mwa Congo wakati wa mashambulizi ya wanamgambo wenye mahusiano na kundi la Islamic State, shirika moja la kiraia la eneo hilo lilisema Ijumaa.
Washambuliaji wa Allied Democratic Forces -ADF walifanya mfululizo wa mashambulizi dhidi ya wenyeji, wakati baadhi walipokuwa wakifanya kazi kwenye mashamba yao, kati ya Jumatano na Ijumaa katika eneo la Mambasa jimbo la Ituri, alisema John Vulverio, mratibu wa New Civil Society of Congo.
Idadi ya waliofariki inasalia kuwa ya muda, kwani hatima ya wengine 20 waliotekwa nyara bado haijulikani, alisema.
Miongoni mwa waliotekwa nyara katika mashambulizi hayo ni mama na dada wa Gilbert Sivayanda, afisa wa serikali ya mtaa, vyombo vya habari vya eneo hilo vilimnukuu mbunge huyo akisema.