Umoja wa Mataifa watoa wito wa kurejeshwa utawala wa kiraia Afrika

Volker Turk, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kibinadamu, akihudhuria Baraza la Haki za Kibinadamu katika Umoja huo huko Geneva, Uswisi Septemba 11, 2023. REUTERS.

Maoni ya Volker Türk yaliweka taswira ya mapema kwa chombo cha juu cha haki za binadamu cha Umoja wa Mataifa wakati akifungua kikao chake cha msimu wa Fall  dhidi ya hali ya mizozo  na migogoro  ikiwa ni pamoja na masaibu ya wahamiaji kutoka Myanmar kwenda Mali na Mexico.

Mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa alitoa wito Jumatatu kufanyika mabadiliko ya haraka kwa mapinduzi ya kijeshi na kurejesha kwa utawala wa kiraia katika nchi za Afrika ambako mapinduzi yamewaondoa madarakani viongozi waliochaguliwa katika miaka ya karibuni huku akishambulia mizozo mingi katika eneo hilo.

Maoni ya Volker Türk yaliweka taswira ya mapema kwa chombo cha juu cha haki za binadamu cha Umoja wa Mataifa wakati akifungua kikao chake cha msimu wa Fall dhidi ya hali ya mizozo na migogoro ikiwa ni pamoja na masaibu ya wahamiaji kutoka Myanmar kwenda Mali na Mexico.

Akizungumzia mzozo wa miaka kumi katika eneo la Sahel ambalo linaenea kote Afrika Kaskazini, katika nchi kama Mali, Burkina Faso na Niger, aliashiria athari za mabadiliko ya hali ya hewa na ukosefu wa uwekezaji katika huduma kama elimu na afya kama sababu ambazo zimechochea misimamo mikali.