'Ulifanya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wetu', Seneta wa Australia amwambia King Charles

King Charles wa Uingereza akiwa katika ziara ya Australia, Oktoba 21, 2024.

Seneta Lidia Thorpe akipinga ziara ya Mfalme wa Uingereza Charles and Malkia Camilla walipohudhuria mualiko wa Bunge huko Canberra, Australia Oktoba 21, 2024.

Thorpe, Seneta aliyechaguliwa kama mgombea huru, na ambaye ni mzawa wa Australia, aliingia kwenye ukumbi huku akipiga kelele na kusema kwamba hatambui ukuu wa mfalme huyo.

Maafisa wa usalama walimzuia kumsogelea mfalme na kutolewa nje ya chumba hicho.

Thorpe, ambaye ameingia kwenye vichwa vya habari siku za nyuma kwa kuwa mwanaharakati wa haki za wazawa, alikuwa mmoja wa watu takriban 20 waliopinga ziara hiyo ya mfalme Charles.