Tillerson aapishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje

Rex Tillerson aapishwa na Makamu wa Rais Mike Pence mbele ya Rais Donald Trump

Rex Tillerson ameapishwa Jumatano usiku kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani masaa machache baada ya kuthibitishwa na Baraza la Seneti.

Makamu wa Rais Mike Pence alimwapisha Tillerson katika ofisi ya Oval ya ikulu ya White House ambako tukio hilo lilishuhudiwa na Rais Donald Trump.

Tillerson alimshukuru Trump kwa kumpa kile alichokiita “nafasi kunjufu,” na kusema kuwa siku zote atayasimamia maslahi ya Wamarekani.