Sudan Kusini: Marufuku ya mitandao ya kijamii yaondolewa

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit. Picha na REUTERS/John Muchucha

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir Mayardit. Picha na REUTERS/John Muchucha

Mamlaka nchini Sudan Kusini imeondoa marufuku ya muda ya mitandao ya kijamii ya  Facebook na TikTok, ambayo iliwekwa wiki iliyopita kufuatia kusambazwa kwa video zilizoonyesha madai ya mauaji ya raia wa Sudan Kusini nchini Sudan.

Picha hizo ambazo zilizua maandamano ya vurugu na mauaji ya kulipiza kisasi kote nchini, zimeondolewa kwenye mitandao ya kijamii, Mamlaka ya Mawasiliano ya Kitaifa ilisema katika barua Januari 27 kwa watoa huduma za mawasiliano na mtandao.

"Kuongezeka kwa ghasia zinazohusishwa na maudhui ya mitandao ya kijamii nchini Sudan Kusini kunasisitiza haja ya kuwa na mtazamo sawia unaoshughulikia sababu kuu za uchochezi wa mtandaoni wakati wa kulinda haki za watu," Napoleon Adok Gai, mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano ya Taifa, alisema katika barua.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yamelilaumu jeshi la Sudan na washirika wake kwa mashambulizi ya kikabila dhidi ya raia katika jimbo la El Gezira nchini Sudan mapema mwezi huu, baada ya kuuteka mji mkuu wa jimbo la Wad Madani kutoka kwa wanamgambo wa kikosi cha RSF.