Sudan inashtumu Umoja wa Falme za Kiarabu kuwasaidia waasi wa RSF

  • VOA News

Balozi wa Sudan kwenye Umoja wa Mataifa, Al-Harith Mohamed akihutubia mkutano wa Baraza la Usalama la UN, Julai 13, 2023. Picha ya AP

“Umoja wa Falme za Kiarabu unapaswa kujiepusha na kuingilia kati masuala ya Sudan,” Balozi wa Sudan, Al-Harith Idriss Al-Harith Mohamed ameliamba Baraza hilo.

“Hili ni sharti la kwanza ambalo litaruhusu uthabiti nchini Sudan. Umoja wa Falme za Kiarabu unatakiwa kusitisha msaada wake kwa RSF,” aliongeza.

Mohamed ameshtumu Umoja wa Falme za Kiarabu kusaidia wapiganaji wa RSF kupitia wanamgambo nchini Chad, Kusini mwa Libya na Afrika ya Kati, akiongeza kuwa Sudan iliwasilisha kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hati kadhaa za kusafiria za Umoja wa Falme za Kiarabu zilizogunduliwa kwenye uwanja wa mapigano mjini Khartoum.

Alisema pia bila kutoa ushahidi kwamba wapiganaji wa RSF waliojeruhiwa wanasafirishwa kwa ndege hadi Dubai ili kupewa matibabu.

Balozi wa Emirati Mohamed Abushabab, ambaye alikuwa amekaa kando ya mwenzake wa Sudan kwenye meza ya wajumbe 15 wa Baraza la Usalama, wakati wa mkutano kuhusu hali nchini Sudan, ameyataja madai hayo kuwa “ya kipuuzi.”