Program ya msaada wa kupambana na Ukimwi inayofadhiliwa na Marekani huenda isiidhinishwe tena

Rais wa zamani George W. Bush alipoadhimisha miaka 20 ya Mpango wa Dharura wa Rais wa Misaada ya UKIMWI barani Afrika, PEPFAR, katika Taasisi ya Amani huko Washington, Feb. 24, 2023.(AP)

Program ya msaada wa kupambana na UKIMWI ya  miaka 20 inayofadhiliwa na Marekani ambayo inasifiwa kwa kuokoa mamilioni ya maisha kote duniani huenda isiidhinishwe tena ikiwa wahafidhina na wanaharakati wanaopinga utoaji  mimba watafanikiwa katika kampeni inayoendelea dhidi yake.

Program ya msaada wa kupambana na UKIMWI ya miaka 20 inayofadhiliwa na Marekani ambayo inasifiwa kwa kuokoa mamilioni ya maisha kote duniani huenda isiidhinishwe tena ikiwa wahafidhina na wanaharakati wanaopinga utoaji mimba watafanikiwa katika kampeni inayoendelea dhidi yake.

Mpango wa dharura wa Rais wa kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) ulizinduliwa mwaka 2003 na Rais wa wakati huo George W. Bush, na tangu wakati huo umetoa zaidi ya dola bilioni 110 kusaidia mapambano dhidi ya janga la UKIMWI katika nchi zaidi ya 50 duniani kote.

Umefanikiwa hasa katika nchi za Magharibi na Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo inasaidia kutoa dawa za kurefusha maisha kwa zaidi ya watu milioni 25 ambao kwa sasa wanaishi na ugonjwa huo.