Papa Francis asema siku ya ukimwi duniani ni  muhimu kuwakumbuka watu walioathirika

Papa Francis yuko kwenye ziwa takatifu la Namugongo.

Papa Francis  alitoa wito wa kuanzishwa upya mshikamano na wale wanaoathiwa na virusi vya UKIMWI ili kuhakikisha huduma kwa wale walio katika maeneo maskini zaidi duniani.

Papa Francis alitoa wito wa kuanzishwa upya mshikamano na wale wanaoathiwa na virusi vya UKIMWI ili kuhakikisha huduma kwa wale walio katika maeneo maskini zaidi duniani.

Akizungumza na hadhira yake, Francis alisema siku ya ukimwi duniani ni siku muhimu ya kuwakumbuka watu walioathirika na virusi hivyo. Katika baadhi ya maeneo ya dunia hakuna upatikanaji wa huduma muhimu, alisema.

UNAIDS, programu ya Umoja wa Mataifa kuhusu VVU na UKIMWI yenye makao yake mjini Geneva, ilisema Jumatatu kwamba janga la COVID-19 lilikuwa likipunguza mapambano na UKIMWI katika maeneo mengi na huduma kwa watu wanaotumia dawa za VVU zilitatizwa katika asilimia 65 ya nchi 130 zilizofanyiwa utafiti.