Mazishi ya Haniyeh yafanyika Doha

Afisa mkuu wa Hamas Khalil al-Hayya, katikati, akiswali mbele ya jeneza la kiongozi wa Hamas aliyeuawa Ismail Haniyeh na mlinzi wake wakati wa sala ya mazishi huko Doha, Qatar, Ijumaa Agosti 2024.

Qatar siku ya Ijumaa imefanya shughuli  za mazishi ya kiongozi wa Hamas Ismail Haniyeh baada ya mauaji yake mjini Tehran, shambulizi lililolaumiwa Israel ambalo limeongeza  hofu ya kuongezeka mzozo wa kikanda.

Haniyeh, mkuu wa kisiasa wa kundi lenye silaha la Palestina, alikuwa akiishi Doha pamoja na wajumbe wengine wa ofisi ya kisiasa ya Hamas.

Amezikwa kwenye makaburi huko Lusail, kaskazini mwa mji mkuu wa Qatar, baada ya swala ya mazishi katika msikiti wa Imam Muhammad bin Abdul Wahhab, ambao ni mkubwa zaidi wa nchi hiyo yenye utajiri wa mafuta.