Mamia waandamana Cape Town  wakipeperusha bendera za Palestina

Maandamano ya kuunga mkono Wapalestina, mjini Cape Town.

Mamia ya watu waliandamana katikati mwa jiji la Cape Town  kuadhimisha mwaka wa kwanza wa mzozo wa Israel na Hamas.

Mamia ya watu waliandamana katikati mwa jiji la Cape Town Jumamosi wakipeperusha bendera za Palestina na kuimba nyimbo dhidi ya Israeli katika maandamano ya kuunga mkono Gaza kuadhimisha mwaka wa kwanza wa mzozo wa Israel na Hamas.

Wakiwa na mabango ya kuishutumu Israel kwa mauaji ya halaiki na ubaguzi wa rangi, waandamanaji hao, wengi wao wakiwa wamevalia skafu ya keffiyeh inayoashiria mapambano ya Wapalestina dhidi ya Israel walitembea hadi bungeni katika maandamano yaliyoandaliwa na Kampeni ya mshikamano wa Palestina.