Mafuriko yaua watu 27 nchini Niger

Mtaa wa mji mkuu wa Niger uliofurikwa, Septemba 3, 2019. Picha ya AFP

Mafuriko nchini Niger yaliyosababishwa na mvua kubwa yaliua watu 27 na kuathiri zaidi ya watu 70, 000 tangu mwezi Julai, maafisa wamesema Jumamosi.

Msimu wa mvua kati ya mwezi Juni na Septemba mara nyingi husababisha mafuriko mabaya katika taifa hilo la Afrika Magharibi lenye jangwa, ikiwemo maeneo makavu ya kaskazini.

Kufikia Agosti 18, mafuriko yalisababisha vifo vya watu 27, kujeruhi watu 30 na kuathiri watu 71,136, wizara ya masuala ya kibinadamu imesema.

Mikoa ya Maradi, Zinder na Tahoua ndiyo iliyoathirika zaidi na nyumba 6,350 ziliporomoka, kulingana na wizara hiyo.

Mji mkuu Niamey, wenye wakazi milioni mbili na tukio la mafuriko mabaya ya mara kwa mara, umenusurika kwa sasa.