Rais Kenyatta azuru pwani ya Kenya.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amekuwa kwenye ziara ya pwani ya nchi, ambako amekuwa akifuatilia miradi ya maendeleo na kujaribu kutatatua migogoro ya umiliki wa ardhi ambayo imekuwa ikisababisha ghasia baina ya jamii tofauti mara kwa mara.

Your browser doesn’t support HTML5

Ziara ya Rais Kenyatta Mombasa.

Serikali inaendelea na zoezi la kutoa hati miliki za mashamba yaliyokua yanamilikiwa na mabwenyenye, lakini hatua hiyo inaonekana na wakosoaji wa serikali kama ya kisiasa.