Ikulu ya Marekani yatoa sababu za kumwalika Rais wa Kenya William Ruto

Rais wa Kenya William Ruto akizungumza wakati wa mahojiano na Reuters kandoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa IDA mjini Nairobi.

Ikulu ya Marekani ilitoa sababu tatu za kumwalika Rais wa Kenya William Ruto siku ya Alhamisi kuvunja kimya kirefu kilichodumu kwa miaka 16 ambapo hakuna kiongozi yeyote wa Kiafrika aliyetuzwa kwa ziara ya kiserikali iliyojaa fahari.

Hizo ni pamoja na imani za kidemokrasia za pamoja za serikali mbili na mtazamo wao sawa katika kutumia sekta binafsi kufikia malengo ya serikali.

Lakini sababu ya msingi, ya sera ya juu ya Afrika ya utawala aliiambia VOA, ni uamuzi wa hivi karibuni wa Kenya kujitangaza duniani kote kwa kutoa askari 1,000 wa kulinda amani Haiti. Ikiwa ni sehemu ya kwanza ya polisi kuwepo nchini Haiti wanatarajiwa kufika huko wiki hii.

Tuliichagua Kenya kwa sababu chache, Frances Brown, mkurugenzi mkuu wa masuala ya Afrika katika Baraza la Usalama wa Taifa, aliiambia VOA wakati wa mahojiano yake ya kwanza na vyombo vya habari tangu achukue wadhifa huo.

Moja ni ushirikiano kati ya Kenya na Marekani kwa kweli umekua kutoka ule unaolenga kanda hadi ule unaolenga kimataifa. Tumefurahishwa sana na jinsi Wakenya wamejitokeza kutekeleza majukumu nje ya kanda yao aliongeza.