China yasisitiza kuwa inatekeleza kikamilifu vikwazo vya Umoja wa Mataifa kwa Korea Kaskazini

Rais Xi Jinping wa China akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 20 la Chama cha Kikomunisti cha China, Oktoba 16,2022. (REUTERS)

China inasisitiza kwamba inatekeleza kikamilifu vikwazo vya Umoja wa Mataifa kwa Korea Kaskazini ikijibu barua kutoka kwenye kundi lijulikanalo Group of Seven, Umoja wa Ulaya na wengine ambao waliitaka Beijing kuizuia Pyongyang kukwepa hatua za vikwazo kwa kutumia maji ya China.

China ilisisitiza siku ya Jumatatu kwamba inatekeleza kikamilifu vikwazo vya Umoja wa Mataifa kwa Korea Kaskazini ikijibu barua kutoka kwenye kundi lijulikanalo Group of Seven, Umoja wa Ulaya na wengine ambao waliitaka Beijing kuizuia Pyongyang kukwepa hatua za vikwazo kwa kutumia maji ya China.

Barua iliyotumwa Ijumaa ilionyesha wasiwasi ikieleza kuhusu kuendelea kuwepo kwa meli nyingi za mafuta zinazotumia maji ya eneo lako katika Sansha Bay kama kimbilio kuwezesha biashara yao ya bidhaa za petroli zilizouliwa kwa Korea Kaskazini.

Ilisainiwa na wanachama wa G7 Marekani, Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan na Uingereza pamoja na Australia, New Zealand, Korea Kusini na Umoja wa Ulaya na imekuja kabla ya ziara ya Korea Kaskazini wiki hii na ujumbe wa ngazi ya juu wa China.