Biden na Trump wajaribu kuwavutia wapiga kura wenye weusi

Your browser doesn’t support HTML5

June 19 hufahamika hapa Marekani kama Juneteenth, sikukuu ya kusherekea kumalizika kwa mfumo wa utumwa katika majimbo 13 ya kusini yaliyofahamika kama Confederate States, yaliyopinga kumaliza kwa mfumo huo na kupelekea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe hapa nchini.

Joe Biden na Donald Trump walitumia siku ya Juneteenth kujaribu kuwavutia wapiga kura weusi wa Marekani ambao wanaonekana wamebadili misimamo yao kuelekea wagombea hao wawili wa kiti cha rais.