Wagombea watatu bora wa CCM watangazwa

Hali nje ya makao makuu ya CCM wakati wa mkutano mkuu 2015

Halmashauri Kuu ya chama tawala cha CCM (NEC), kimemaliza kikao chake mjini Dodoma Juammosi usiku na kuteua majina ya wagombea watatu bora wanaotaka kugombania kiti cha rais kwa niaba ya chama hicho.

Majina hayo yanajadiliwa kwa wakati huu katika Mkutano Mkuu wa chama, ambao jina moja pekee litachaguliwa. Wagombea walotajwa ni Dkt. John Magufuli, Dkt Aisha Rose Migiro na Balozi Amina Salum Ali.

Your browser doesn’t support HTML5

Uchambuzi juu ya uteuzi wa mgombea wa CCM

Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nuauye, wagombea waloachwa Bernard Membe na January Makamba wamekubali na kupokeya matokeo na kusema kuwa wako tayari kumunga mkono mgombea yeyote atakayechaguliwana mkutano mkuu.