Mahojiano ya Profesa Mwesiga Baregu na Sauti ya Amerika

Your browser doesn’t support HTML5

Rais Jakaya Kikwete ambaye ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania, amesema mgombea Urais wa chama chake bado hajajitokeza, licha ya kuwepo wanachama wanaoonyesha nia ya kugombea nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu wa mwezi Desemba. Kufuatia kauli ya Bwana Kikwete, Idd Ligongo wa Idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika alifanya mahojiano na Profesa Mwesiga Baregu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino juu ya kauli ya Rais Kikwete aliyoitoa katika maadhimisho ya miaka 38 ya CCM.