Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 03, 2025 Local time: 01:21

Zaidi ya wahamiaji laki 5 wa Haiti kupoteza vibali vya kuishi Marekani


Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani, Kristi Noem, akiwa kwenye Ikulu ya Marekani.
Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani, Kristi Noem, akiwa kwenye Ikulu ya Marekani.

Waziri wa Usalama wa Ndani wa Marekani Kristi Noem Alhamisi amepunguza muda wa kulinda wahamiaji dhidi ya kurejeshwa pamoja na kufuta vibali vya kufanya kazi kwa wahamiaji 521,000 wa Haiti waliokuwa chini ya mpango maalumu ikiwa na maana kwamba utamalizika Agosti, msemaji wa wizara hiyo amesema.

Tangazo hilo sasa linabatilisha hatua ya utawala wa Biden mwaka jana ya kuongeza muda wa program hiyo hadi Februari 2026, msemaji huyo amesema, akiongeza kuwa hatua hiyo haikuwa muhimu. Rais Donald Trump ambaye ni Mrepablikan wakati wa muhula wake wa kwanza kati ya 2017- 2021 alijaribu kumaliza program hiyo ambayo pia inajulikana kama TPS, lakini alizuiliwa na mahakama za serikali kuu.

Mapema mwezi huu Noem alifuta program hiyo kwa raia 600,000 wa Venezuela, wakati nusu yao wakipoteza vibali vya kufanya kazi. Zaidi ya watu milioni 1 zaidi ya nusu wakiwa watoto wamekosehwa makazi ndani ya Haiti ambako ghasia za magenge zimeshamiri licha ya juhudi za Umoja wa Mataifa za kutumia walinda usalama mwaka uliopita, data za Umoja huo zilizochapishwa Januari zinaonyesha. Tangu 2023, Haiti haijakuwa na viongozi wa kuchaguliwa na wala haijafanya uchaguzi tangu 2016.

Forum

XS
SM
MD
LG