Shambulio la Alhamisi la bunduki na maguruneti ya kurushwa kwa roketi pia liliwajeruhi maafisa wanane. Lilifanyika katika eneo la Kacha katika wilaya ya Rahim Yar Khan, ambalo linajulikana kwa maficho kando ya Mto Indus ambapo mamia ya majambazi wenye silaha nzito huwakwepa polisi.
Mkuu wa polisi wa Punjab Usman Anwar alisema polisi walimuua kiongozi wa majambazi ambaye alikuwa akihusika na shambulio hilo. Katika taarifa yake, alisema operesheni dhidi ya majambazi hao bado inaendelea, na itaendelea hadi jambazi wa mwisho atakapoondolewa mkoani humo.
Forum