Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Septemba 12, 2024 Local time: 21:02

WHO yasema Mpox inaweza kutokomezwa


Shirika la Afya Duniani (WHO) linaripoti kwamba hatua za kimsingi za afya ya umma zinaweza kukabiliana na milipuko ya mpox na uwezekano wa kuondoa maambukizi ya virusi, ambavyo vimesababisha maambukizi 99,176 na vifo 208 dunia nzima toka 2022.

“Tunajua jinsi ya kudhibiti mpox, na ukanda wa Ulaya, zinahitajika juhudi kukomesha maambukizi,” Dkt Hans Kluge, mkurugenzi wa kanda ya Ulaya ya WHO, amewaambia wanahabari Jumanne mjini Geneva.

Amesema miaka miwili iliyopita mpox ilidhibitiwa Ulaya, kutokana na ushirikiano wa moja kwa moja na jumuiya zilizoathirika zaidi za wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja baada ya kufanya uchunguzi wa kina pamoja kutoa ushauri mzuri wa afya ya umma.

Akizungumza kwa njia ya video kutoka Copenhagen, Kluge amesema WHO iliweza kudhibiti mlipuko huo kupitia mabadiliko ya tabia na hatua zisizo za kibaguzi za afya ya umma, pamoja na chanjo ya mpox.

Forum

XS
SM
MD
LG