Meya Terekhov, amesema huenda bado kuna watu chini ya vifusi kufuatia shambulizi katika mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine.
Kharkiv na mji jirani kwa muda mrefu imelengwa na mashambulizi ya Russia, lakini kwa siku za karibuni mashambulizi yamekuwa makali zaidi yakiwalenga raia na mtandao wa nishati wa eneo hilo.
Russia, inakanusha kuwalenga raia kwa makusudi, lakini maelfu ya raia tayari wameuwawa na kujeruhiwa katika kipindi cha uvamizi wake kwa Ukraine.
Forum